Klabu ya Simba imemrejesha kocha Juma Mgunda kwenye timu ya wanawake 'Simba Queens' baada ya kumtoa katika benchi la ufundi la Simba SC ya wanaume
Hii ni baada ya Simba kumtoa Mgunda katika Benchi la Ufundi la timu ya wanaume kufuatia ujio wa kocha Fadlu Davids raia wa Afrika Kusini aliyetua na wasaidizi wake wanne.
Mgunda alirejea kwenye kikosi cha wanaume kama kaimu Kocha Mkuu wakati msimu ukielekea mwisho baada ya kuondoka kwa aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Abdelhak Benchikha raia wa Algeria ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha Jeunesse Sportive de Kabylie, maarufu kama JS Kabylie ama JSK.