Kocha wa zamani wa Simba Queens, Mussa Hassan Mgosi amesema usajili wa wachezaji wa kigeni unakidhi mahitaji ya klabu kuleta ushindani, lakini kwa timu ya taifa inakuwa ngumu.
Akichangia mjadala ulioandaliwa kwenye mtandao wa X na kampuni ya Mwananchi Communications Limited Mgosi amesema inatakiwa kifanyike kitu kwenye timu ya taifa ili iwe na nguvu, akisisitiza wachezaji 12 wanaosajiliwa wanaruhusiwa kucheza wote tofauti na zamani walisajiliwa sita walicheza watatu ambao wazawa walipata nafasi.
Mgosi huo ni mjadala mpana kwasababu unagusa taifa, akishauri kunatakiwa kutafutwe namna ya kuboresha jambo hilo kwa maslahi ya timu ya Stars.
Timu za wanawake ameona wasajiliwa wachezaji wa kigeni angalau watano, watatu wacheze, wawili wasubili ili kulijengea nguvu soka hilo.