Wed, 21 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa Timu ya Taifa ya Guinea ya Ikweta, Emilio Nsue ametangaza kustaafu soka la kimataifa akiwa na umri wa miaka 34.
Nsue ambaye anachezea klabu ya Intercity ya Uhispania alikuwa mfungaji bora wa michuano ya kombe la Mataifa Afrika AFCON 2023 akiwa na magoli matano.
Nsue ameichezea Equatorial Guinea mechi 42 huku akipachika jumla ya magoli 23.
Hatua hiyo ya Nsue imekuja siku chache baada ya kuibuka sintofahamu baina yake na Chama cha Soka cha Equatoria Guinea na kupelekea kusimamishwa Timu ya Taifa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live