Leo Julai 11 Yanga wametangaza usajili wa beki Fred Gift Raia wa Uganda kutoka kalabu ya SC Villa ya Uganda.
Huu ni usajili wa pili kwa Klabu ya Yanga baada ya ule wa Nickson Kibabage alietokea Singida Fountain Gate.
Tanzaniaweb Tunakuletea Wasifu (CV) Kamili ya Usajili huo wa Wananchi;
Beki bora wa Uganda 2022/23 Pulse award, beki bora namba 2 wa ligi kuu Uganda (2022/23),
Pia ametajwa kwenye kikosi bora cha msimu Uganda 2022/23 na mchezaji wa timu ya Taifa ya Uganda , Gift Fred kutoka SC Villa,
Jina - Fred Gift
Uraia- Uganda
Amezaliwa- 21 July 1998 (24 yrs)
Urefu - 1,84 m (Futi 6.1in)
Nafasi- Centre-back
Mguu anaotumia - Right footer (70 kg)
Fred amekulia katika akademi ya chuo kikuu cha Uganda, kinachoitwa Bugema University.
Ukiacha soka na uwezo mkubwa kwenye soka lake pia Fred pia ni msomi, ana Degree , amesomea masuala ya Information Technology (IT).
Fred alichaguliwa kuwa Beki bora wa Uganda (2019) akiwa katika timu ya Chuo, Bugema University kwenye mashindano ya Vyuo Vikuu Nchini Uganda,
2020 - Fred alisajiliwa na klabu ya Gomba Lions, akafanikiwa kutwaa kombe la The Masaza cup, akachaguliwa pia kuwa beki bora wa msimu wa mashindano hayo.
2021 alisajiliwa na klabu ya SC Villa kwa Mkataba wa miaka (3), Msimu wa 2021/22 alichaguliwa kwenye kikosi bora cha ligi kuu ya Uganda,
Fred ni Nahodha wa SC Villa.
Msimu wa 21/22 - Fred akiwa Sports Club Villa
Michezo- 26
Magoli - 2
Kadi za njano- 1
Kadi nyekundu- 0
Mchezaji bora Villa
Kikosi bora ligi kuu
Msimu wa 22/23 | Fred akiwa Villa
Michezo- 27
Magoli- 2
Kadi za njano- 2
Kadi nyekundu- 0
Kikosi bora ligi kuu ✔️ Runer-up beki bora ✔️
Moja ya sifa zake Mlinzi huyo
Kasi
Nguvu
Maarifa
Nidhamu / Msikivu
Control
Kikosi bora cha Uganda 2022/2023.
S. Tamale (Maroons)
Matsiko Grant (Wakiso Giants)
Denis Kaka (B stars)
Gift Fred (SC Villa)
Mukundane (Vipers)
Bukenya Laurence (Wakiso)
G. Wahab (Arua Hill)
L. Tibita (Busoga)
Milton Karisa (Vipers)
B. Baale (SC Villa)
Kayiwa (Express)
Gift ni nahodha wa klabu ya SC Villa, pia anauwezo Mkubwa sana kuchez nafasi zote za Ulinzi Uwanjani, Yaani beki zote 2,3,4 na 5
Gift Fred anakwenda kuwa mbadala wa Doumbia au Djuma ambao wanatajwa kuoneshwa mlango wa kutokea.
Pia upo uwezekano wachezaji wote hao kuachwa / kutolewa kwa Mkopo.