Timu ya Taifa ya Mexico imeshinda kombe la kombe la dhahabu la CONCACAF (CONCACAF Gold Cup) 2023 kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Panama katika dimba la SoFi Los Angeles, Marekani kwenye FAINALI.
FT: Mexico 1-0 Panama
⚽ Santiago Gimenez 87'
Mexico imetwaa kombe Gold Cup kwa mara ya 9 ikiwa ndio Taifa lililotwaa taji hilo mara nyingi kuliko katika historia ya michuano ya CONCACAF. Marekani imetwaa mara 7 huku Canada ikitwaa mara moja.
SAFARI YA TIMU HIZI KWENYE CONCACAF GOLD CUP 2023
Mexico ilitinga fainali baada ya kuzifunga Honduras 4-0 na Haiti 3-1 lakini ikipoteza 1-0 dhidi ya Qatar kwenye kundi B, kabla ya kuitandika Costa Rica 2-0 kwenye robo fainali na kuiondosha Jamaica 3-0 kwenye nusu fainali.
Kwa upande wa Panama ilizifunga Costa Rica 2-1, Martinique 2-1 na kutoka sare ya 2-2 dhidi ya El Salvador kwenye kundi C, kabla ya kuikanda Qatar 4-0 kwenye robo fainali na kuiondosha Marekani kwa matuta 5-4 kwenye nusu fainali.
NB: Qatari imealikwa kwenye michuano ya Gold Cup 2021 na 2023 kama sehemu ya ushirikiano kati ya CONCACAF na Shirikisho la Soka la Qatar (QFA).