Kipa wa Singida Big Stars, Metacha Mnata amefungiwa mechi tatu kutozwa faini ya Tsh milioni moja kwa kosa la kumpiga kwa makusudi mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Charles Ilanfya wakati wa mchezo kati ya Timu hizo.
Kipa wa Singida Big Stars, Metacha Mnata amefungiwa mechi tatu kutozwa faini ya Tsh milioni moja kwa kosa la kumpiga kwa makusudi mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Charles Ilanfya wakati wa mchezo kati ya Timu hizo. Mechi hiyo ilichezwa mnamo Oktoba 18, 2022 Mtibwa Sugar ikiibuka na ushindi wa 1-0 huku Ilanfya akifunga bao hilo pekee katika dimba la Manungu Complex, Turiani Morogoro.