Wed, 18 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Argentina na Klabu ya Inter Miami, Lionel Messi tayari ametawazwa kuwa mshindi tuzo ya Ballon d'Or 2023, licha ya kutotangazwa.
Kwa mujibu wa ukurasa wa Michezo Goalglobal Messi atatangazwa kama mchezaji Bora wa Dunia baada ya kuiwezesha Argentina kutwaa Kombe la Dunia huko Qatar 2022.
Tayari nyota huyo ameshinda tuzo hiyo ya Dhahabu mara saba. Messi anakuwa mchezaji wa kwanza kushinda mara nyingi tuzo hiyo.
Messi pia atakuwa mchezaji wa kwanza kupokea tuzo hiyo akiwa anacheza soka lake nje ya Ulaya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live