Mon, 22 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa klabu ya Inter Miami inayoshiriki nchini Marekani Leonel Messi amebakiza magoli 10 pekee ili aweke rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo.
Hadi hivi sasa Messi amecheza michezo 23 akiwa amefunga magoli 20, anayeshikiria rekodi hiyo ni Gonzalo Higuain aliye na magoli 29 katika michezo 70 na ameshastaafu soka.
Aliye nafasi ya pili ni Leonardo Campana ambaye bado anacheza klabuni hapo akiwa na magoli 25 katika michezo 73 aliyocheza.
Ligi ni rahisi au Messi ndio anajua kupita wote
Chanzo: www.tanzaniaweb.live