Nyota wa ‘timu’ ya Taifa ya Argentina na ‘klabu’ ya Inter Miami kutoka Marekani, Lionel Messi ameibuka kinara kwa kuwa ndiye mchezaji aliyetafutwa zaidi kupitia mitandao ya kijamii kwa mwaka 2023.
Kwa mujibu wa tovuti ya FBref inayojihusisha na takwimu za michezo imeripoti kuwa Messi ndiye mchezaji aliyetazamwa na kufuatiliwa mara nyingi katika mitandao ya kijamii kwenye nchi tofauti kwa mwaka huu huku Cristiano Ronaldo akishika namba moja Ureno pekee.
Aidha wana-soka wengine ambao wameshika namba moja kwenye mataifa yao ni #Neymar, Mbappe, Vinicius Jr, Guti na mchezaji wa Chelsea, Moisea Caicedo.