Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Messi amshangaza Rais FC Barcelona

Image 494 1140x640.png Messi amshangaza Rais FC Barcelona

Sat, 29 Jul 2023 Chanzo: Dar24

Rais wa FC Barcelona, Joan Laporta ameiambia ESPN ni hisia ya ajabu kumuona Lionel Messi akiwa na jezi ya Inter Miami CF, lakini akamtakia Mshambuliaji huyo kila la heri kwenye Ligi Kuu ya soka ya Marekani, MLS.

Messi mwenye umri wa miaka 36 aliondoka FC Barcelona na kwenda Paris Saint-Germain miaka miwili iliyopita, lakini timu hiyo ya Katalunya ilijaribu kumsajili tena mapema msimu joto wakati mkataba wake na timu hiyo ya Ufaransa ilipokwisha.

Timu ya Saudi Arabia Al-Hilal pia ilimpa Messi mkataba, lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina aliamua kujiunga na Inter Miami, ambapo amefunga mabao matatu katika mechi zake mbili za kwanza.

“Ni hisia ngeni,” Laporta aliiambia ESPN kuhusu kumtazama Messi akicheza Marekani.

“Tulimtambulisha Messi na Barcelona. Hivyo ndivyo ninavyofikiri mashabiki wengi wanamwona Messi, kwa sababu muda mwingi wa soka yake amekuwa Barca.

“Lakini tunaheshimu uamuzi wake na tunamtakia mema. Tunawatakia mema wachezaji wetu. Alikuja Barcelona akiwa mtoto, mwenye umri wa miaka 14, na alikaa nasi kwa miaka 20. Natumaini anaweza kuwa mzuri sana.”

Messi tayari ameunganishwa Miami na wachezaji wenzake wa zamani wa Barca Sergio Busquets na Jordi Alba, huku Luis Suarez pia akihusishwa, ingawa vyanzo vimeiambia ESPN mshambuliaji huyo wa Uruguay atabakia Gremio hadi angalau mwisho wa mwaka.

Laporta alisema anaelewa uamuzi wa Messi kuchukua changamoto mpya nchini Marekani, hata kama Barca wangeondoa uwezekano wake wa kurejea La Liga.

Chanzo: Dar24