Wed, 23 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa Inter Miami raia wa Argentina Lionel Messi amesema kwa sasa hachezi soka akiwa na kiu ya kushinda mataji.
Messi amesema tayari ameshashinda kila kitu ambacho mwanasoka anakihitaji katika maisha yake ya Soka kuanzia ngazi ya Klabu mpaka Timu ya Taifa.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Messi anasema;
“Hakuna ninachodaiwa katika mpira wa miguu, nimemaliza kila kitu. Kwa Sasa nacheza Kama kujifuraisha tu"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live