Mshambuliaji wa Klabu ya PSG na Timu ya Taifa ya Argentina Leonel Messi amefunguka kuwa baada ya kushinda taji la Kombe la Dunia alipokea jumbe nyingi kupitia ukurasa wake wa Instagram mpaka kupelekea Instagram kuifungia akaunti yake kwa muda
"Akaunti yangu ya Instagram ilifungiwa kwa muda kutokana na kupokea jumbe nyingi", Messi ameiambia ESPN
Jambo lingine ambalo Messi amefunguka ni kuhusiana na uendeshaji wa akaunti yake ya Instagram.
Messi amesema kuwa anaendesha mwenyewe akaunti yake ya Instagram wala sio kampuni kama wanavyofikiri kwa hiyo chochote utakachokiona kwenye ukurasa wake jua ni yeye mwenyewe ame post.