Fri, 23 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Medeama imezishutumu Al Ahly na CR Belouizdad kuwa zinatumia mbinu ili kuwachafua huku klabu hiyo ikiipongeza Yanga SC kujitofautisha na klabu hizo mbili.
Medeama wameweka wazi kuwa Al Ahly mbinu yao waliyotumia ya kutoa taarifa kuwa ndege yao ilipata hitilafu hivyo wameomba mchezo kusogezwa mbele, CR Belouizdad pia iliwahi kuripoti kuwa ndege yao binafsi ilizuiliwa kutua.
Medeama wamesema hakuna timu yoyote itakayosikilizwa na CAF kwenye hili, na mchezo huo wamesisitiza utapigwa leo Ijumaa kama ilivyokuwa imepangwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live