Fri, 15 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Makamu wa Rais wa Yanga SC, Arafat Haji amesema, kwenye mechi za Kimataifa, utani wa Simba na Yanga unapaswa kuwekwa kando.
“Watu wanaofuatilia mpira wa miguu na kufuatilia derby ya Tanzania pengine na wao wanatamani kuona derby ya Tanzania inacheza fainali ya Champions League “
“Tunatamani kuweka historia ya kulibeba kombe kwa timu ya hapa nyumbani ,uzuri tunapokwenda kwenye mambo ya kimataifa utani unatakiwa kukaa pembeni”
“Utani ni urithi wetu na ndio maana msimu huu tumekuja na huo msemo wa utani uwe na faida kwetu."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live