Baada ya Ligi ya NBC kurejea kutoka kwenye mapumziko kupisha Fainali za AFCON 2023, Tanzania Prisons ni miongoni mwa timu ambazo zimekusanya alama nyingi ukizitoa timu tatu za juu kwenye msimamo wa Ligi [Yanga, Azam na Simba].
Timu nyingine ambazo zimekusanya alama nyingi baada ya Ligi Kuu kuendelea ni Coastal Union, Tanzania Prisons, Kagera Sugar, Ihefu na Mashujaa FC.
Tanzania Prisons imekusanya alama 10 kwenye michezo mitano iliyopita [imeshinda miechezo mitatu, imetoka sare mchezo mmoja na kupoteza mchezo mmoja].
❌ Tanzania Prisons 1-2 Yanga ✅ Tanzania Prisons 3-1 Singida Fountain Gate FC ???? Tanzania Prisons 1-1 Azam FC ✅ Tanzania Prisons 2-1 Tabora United ✅ Simba 1-2 Tanzania Prisons
Katika michezo hiyo mitano, michezo mitatu ilikuwa dhidi ya timu zinazowania ubingwa msimu huu [Yanga, Azam na Simba], ni Yanga pekee ndio ilifanikiwa kuondoka na alama tatu. Azam iliondoka na alama moja, Simba imeacha alama zote tatu.