Tue, 23 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya wenyeji JKT Tanzania dhidi ya Bingwa mtetezi Yanga umeahirishwa.
Hatua hiyo imekuja baada ya Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni Jijini Dar es Salaama kujaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar.
Kamisaa wa Mchezo huo, Kamwanga Tambwe ndio alietoa taarifa hiyo kwa ufupi huku akisema kuwa wanaendelea kufanya mawasiliano ili kufanya maamuzi na kuujulisha Umma tarehe rasmi ya mchezo huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live