Wed, 28 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa zamani wa Arsenal Kristoffer Olsson amegundulika na ugonjwa mkali wa ubongo mara baada ya kuanguka na kupoteza fahamu akiwa nyumbani kwake wiki iliyopita.
Olsson (28) raia wa Sweden yupo kwenye mashine ya kumsaidia kupumua, klabu yake ya FC Midtjylland ya nchini Denmark imethibitisha leo.
Kiungo huyo aliichezea klabu ya Arsenal kwa miaka mitatu na kuondoka mwaka 2014. Amewahi pia kucheza soka nchini Ubelgiji, Sweden na Urusi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live