Wakati Historia ya Ligi ya Mabingwa ikiwataja nyota wengi kama Lionel Messi, Cristiano Ronaldo nk wakionekana kufanya makubwa.
Legend wa Man United, Rio Ferdinand amesema jambo kuhusiana na nyota Clarence Seedorf;
"Kwangu mimi Clarence Seedorf ndiye mchezaji asieongelewa sana katika historia nzima ya Ligi ya Mabingwa.
Jamaa huyu ameshinda kombe hili mara 4 akiwa na vilabu 3 tofauti. Alikuwa , Mwenye nguvu, mwenye kasi na anaweza kubadilisha kasi ya mchezo mda wowote.
Lakini hakuwahi kuchukuliwa kama nyota bora."
Seedorf amewahi kubeba Ubingwa wa Ulaya akiwa na vilabu vya Ajax, Real Madrid na AC Milan.