Shirikisho la soka la Uturuki limethibitisha kuwa klabu ya Trabzonspor itacheza mechi zao sita zijazo za nyumbani bila mashabiki huku wachezaji wawili wa Fenerbahce wakifungiwa mechi moja kutokana na rabsha wakati timu hizo zilipokutana.
Shirikisho la soka la Uturuki limethibitisha kuwa klabu ya Trabzonspor itacheza mechi zao sita zijazo za nyumbani bila mashabiki huku wachezaji wawili wa Fenerbahce wakifungiwa mechi moja kutokana na rabsha wakati timu hizo zilipokutana. Bright Osayi-Samuel , ambaye alishambuliwa na shabiki uwanjani na kuonekana akipambana na shabiki huyo ili kujiokoa, hajapewa adhabu yoyote.