Tue, 7 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa klabu ya Richards Bay ya Ligi kuu Afrika Kusini, Siphamandla ‘Spepe’ Mtolo amefariki Dunia leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 29 klabu hiyo imethibitisha.
Mtolo almaarufu ‘Spepe’ ambaye alikuwa anacheza nafasi ya kiungo mkabaji alianguka wakati wa mazoezi ya klabu hiyo leo asubuhi hali iliyopelekea umauti kumkuta.
Mtolo aliichezea Richards Bay FC dakika zote 90 katika kipigo cha 1-0 cha klabu hiyo dhidi ya klabu ya Kaizer Chiefs Weekend.
Hii hapa taarifa kamili ya Klabu;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live