Straika wa kimataifa wa Ghana Raphael Dwamena amedondoka ghafla uwanjani na kufariki wakati anaitumikia timu yake KF Egnatia kwenye mchezo wa Ligi Kuu Albania dhidi ya Partizani leo Jumamosi.
Baada ya kudondoka staa huyu alipatiwa huduma ya kwanza kiwanjani hapo kisha akakimbiziwa hospitali lakini ilishindikana kumuokoa na akapoteza maisha licha ya jitihada zilizofanywa na madaktari.
Licha ya kuwa mmoja kati ya wachezaji walioonekana kuwa na kiwango bora, Dwamena muda wake mwingi wa maisha yake ya soka aliutumia nchini Austria na kwa kiasi kikubwa kiwango chake kiliathiriwa na matatizo ya moyo yaliyokuwa yanamsumbua.