Mon, 8 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa AS Kigali na timu ya taifa ya Rwanda amefariki Dunia baada ya kugongana na golikipa uwanjani.
Jean Paul Ahoyikuye alikuwa anafanya mazoezi na marafiki zake wa mitaani katika mchezo wa kujiweka vizuri kutokana na Ligi Kuu kumalizika.
Taarifa zinasema kuwa mchezaji huyo wa AS Kigali alimeza ulimi baada ya kugongana na golikipa ambapo alifariki Dunia wakati anakimbizwa katika hospitali ya CHUK.
Kabla ya kuitumikia AS Kigali aliwahi pia kuichezea timu ya Kiyovu Sports zote za Ligi Kuu nchini Rwanda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live