Timu ya Soka ya Tanzania Prisons ya Jijini Mbeya imeingia udhamini na kampuni ya Bens Agrostar kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi Million 150 ambao una kipengele cha kuboresha mkataba.
Timu ya Soka ya Tanzania Prisons ya Jijini Mbeya imeingia udhamini na kampuni ya Bens Agrostar kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi Million 150 ambao una kipengele cha kuboresha mkataba. Agrostar wamesema kwa nyongeza wanatoa Ahadi ya Million 10 kama timu hiyo itaibuka na ushindi katika mchezo dhidi ya Simba ama Yanga, na pia wanafikiria mwisho wa msimu mchezaji bora wa klabu aweze kujengewa nyumba.