Thu, 2 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kuipandisha Daraja la Ligi Kuu Tanzania Bara kikosi cha timu ya Pamba Jiji kocha wa kikosi hicho Mbwana Makata ameweka rekodi ya kuwa kocha aliyewahi kuzipandisha Daraja timu nne ndani ya miaka saba.
Kocha Makata amewahi kuzipandisha daraja timu za Alliance FC: 2017/2018, Polisi Tanzania: 2018/2019, Dodoma Jiji FC: 2019/2020 na Pamba Jiji FC: 2023/2024.
Kocha mwingine aliyekuwa na sifa ya kuzipandisha daraja timu kutoka Daraja la Kwanza kuja Ligi Kuu ni Hayati Hassan Banyai.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live