Kiungo mshambuliaji wa Singida Fountaine Gate, Bruno Gomes amerejea nchini tayari kwa safari ya Tanga akijiandaa kuikabili Simba katika Ngao ya Jamii.
Bruno alikuwa nchini kwao Brazil kwa mapumziko na ametua tayari kwa msimu mpya akiwa na waajiri wake Singida FG.
Kwa upande mwingine Kocha Mkuu wa Singida, Hans Van Pluijm amesema
“Wachezaji wangu wamenionyeshea namna walivyo tayari kwa michezo ya ushindani, tuna mchezo dhidi ya Simba hivi karibuni, naamini tupo tayari kukabiliana nao kutokana na ubora wa wachezaji wangu, walioangalia mchezo wetu na As Vita wanaweza kuona namna kikosi kilivyoimarika,"