Mon, 6 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watoza Ushuru wa Jiji la Mbeya, Timu ya Mbeya City wameibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Mabao ya Mbeya City leo yamefungwa na Hussein Masalanga dakika ya 42 na Paul Nonga dakika ya 88.
Kwa ushindi huo timu hiyo inafikisha pointi 14 na kupanda nafasi ya tatu, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake12 ikishukia nafasi ya tano baada ya wote kucheza mechi nane.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live