Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbappe yeye na Real Madrid tu

Mbappe Kiburi Kylian Mbappe

Thu, 12 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mmoja wa wajumbe wa Klabu ya Real Madrid ametoa siri kuwa Mshambuliaji wa Paris St-Germain na Ufaransa, Kylian Mbappe anataka kujiunga na timu yao katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi wakati mkataba wake wa sasa utakapomalizika.

Mbappe mwenye umri wa miaka 24, mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwakani na amegoma kusaini dili jipya.

Mbappe ambaye msimu huu amecheza mechi tisa za michuano yote na kufunga mabao manane, anahitajika pia na baadhi ya timu barani Ulaya.

Staa huyu wa kimataifa wa Ufaransa aliingia kwenye mgogoro na mabosi wa PSG baada ya kugoma kusaini kipengele cha kuurefusha mkataba wake kufikia mwaka 2025.

Mbali ya Madrid, saini ya Mbappe pia imekuwa ikiwindwa na baadhi ya vigogo nchini Saudi Arabia lakini yeye mwenyewe mpango wake zaidi kutua nchini Hispania.

Hadi sasa viongozi wa PSG wameendelea kushikilia msimamo wa kutotaka kumuachia Mbappe na bado wana matumaini ya kwamba atasaini mkataba wa kuendelea kusalia kwenye timu yao kabla ya msimu huu kumalizika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live