Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji kinda wa Tanzania anayekipiga KRC Genk ya nchini Ubelgiji, Kelvin Pius John (20) ameendelea kung’aa katika ligi ya vijana nchini humo baada ya jana kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 5-1.
Genk U - 23 ilicheza dhidi ya Royal Francs-Borains U - 20 na Kelvin akifunga bao moja na kutengeneza bao lingine moja.
Bao hilo la Kelvin limemfanya afikishe idadi ya mabao mawili katika ligi hiyo na kuwa kinara wa upachikaji mabao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live