Tue, 16 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Kifaransa, Kylian Mbappé amekamilisha vipimo vya afya huko Real Madrid na sasa mipango ya kutambulishwa kwake kama mchezaji mpya wa Mabingwa hao wa Ulaya inaendelea.
Leo ndio siku ya utambulisho wa nyota huyo raia wa Ufaransa baada ya kutoka amesaini jezi (autograph) za baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo ambao walikuwa hapo kumsubiri nyota wao huyo mpya.
Utambulisho wa Mbappe ambaye ametokea PSG utashuhudiwa na mashabiki 85,000 katika uwanja wa nyumbani wa klabu hiyo, Santiago Bernabeu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live