Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbappe akanusha kumdhihaki Neymar amta Uwanjani haraka

Mbappe X Naymar Mbappe na Neymar

Mon, 20 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kylian Mbappe amesisitiza kuwa hakuwa akitoa maoni yake dhidi ya Neymar alipowataja wachezaji wenzake wa klabu ya Paris Saint-Germain kuwa lazima kula vizuri na kulala vizuri.

Mbappe alikuwa mmoja wa magwiji wa PSG siku ya jana waliponyakua ushindi wa 4-3 dhidi ya Lille kwenye mechi ya kusisimua ya Ligue 1.

Neymar alifunga bao la pili na kufanya 2-0 kwa wenyeji Parc des Princes ndani ya dakika 17, lakini mchezaji huyo wa Brazil alitoka nje akiwa na jeraha kubwa la kifundo cha mguu mapema kipindi cha pili huku Lille wakirekebisha mzani na kisha kuongoza.

Bado Mbappe aliikokota PSG, hivyo kumtengenezea mazingira Lionel Messi kushinda kwa mkwaju wa faulo hadi dakika za lala salama, na hivyo kuhitimisha ushindi wa mechi tatu mfululizo kwa PSG, ambao walikuwa nyuma kwa bao 1-0 katika mchezo wao wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Bayern Munich.

Mbappe aliwataka wachezaji wenzake kutunza utimamu wao na viwango vyao vya nishati kabla ya mechi ya mkondo wa pili Machi 8, lakini siku moja baadaye Neymar alipigwa picha kwenye tawi la McDonald usiku wa kuamkia Paris.

Christophe Galtier alifichua katika maandalizi ya mechi ya jana kwamba alijadili suala hilo na Neymar, lakini Mbappe alisisitiza kwamba maoni yake hayakuwa na maana ya kumpinga supastaa mwenzake.

Mbappe amesema; “Niliona kwamba watu walikuwa wakizungumza kuhusu Ney, kuhusu kile kilichotokea. Hayakuwa maoni dhidi ya Neymar. Katika muktadha, tunahitaji kila kitu isipokuwa mapigano. Ni ushauri kwa kila mtu.”

Kylian aliongeza kuwa anatumai Neymar atarejea hivi karibuni kwa sababu ni mchezaji muhimu kwao.

Kuonekana kwa Neymar akitolewa kwenye machela hakukuwa na matumaini kwa PSG, na Galtier alisema, pengine ni kifundo cha mguu, tutaona uzito wake kwani anachunguzwa.

Mechi ilikuwa muhimu sana kwa kila mtu, kwa wachezaji, kwangu. Tulijua kwamba ushindi ulikuwa wa lazima ili kuweka upya nguvu. Alisema Galtier.

“Kocha ambaye anapoteza mechi nne mfululizo, hata zaidi akiwa PSG, ni wazi yuko kwenye ugumu, kunaweza kuwa na shaka. Ninachoweza kukuambia ni kwamba ninaungwa mkono wa kudumu na usimamizi wangu wa michezo na rais wangu. Ni muhimu sana.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live