Thu, 27 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa PSG Kylian Mbappe amekataa kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Al Hilal juu ya uwezekano wa Mfaransa huyo kujiunga na miamba hiyo ya Saudi Arabia.
Nyota huyo wa zamani wa Monaco hana mpango wa kuanzisha mazungumzo na Al Hilal licha ofa nono ya mshahara wa Euro milioni 200.
PSG inaamini Mfaransa huyo amedhamiria kujiunga na Real Madrid na inaripotiwa kuwa tayari amefanya makubaliano ya siri na Mabingwa hao wa kihistoria wa Ligi ya Mabingwa Ulaya juu ya kujiunga nao mwishoni mwa msimu ujao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live