Nyota wa kimataifa wa Ufaransa na PSG, Kylian Mbappe ameweka wazi kuwa hana mpango wa kuondoka ndani ya miamba hiyo ya Ufaransa na kusisitiza kuwa haendi popote pale.
Mbappe ameyasema hayo kwenye mahojiano baada ya mchezo wa nusu fainali ya UEFA dhidi ya Barcelona ambapo PSG iliibuka na ushindi wa mabao 4-1 huku Mbappe akifunga mabao mawili.
"Mchezo huu hautabadilisha uamuzi wangu juu ya siku zijazo, Kylian Mbappé alipoulizwa kama ushindi dhidi ya Barcelona unaweza kubadilisha uamuzi wake kwa siku zijazo: "Hapana, hapana, hapana...".
"Ninajivunia kuivaa jezi ya PSG, mimi ni Parisien na nina ndoto ya kushinda Ligi ya Mabingwa na PSG".