Tetesi za usajli kutoka nchini Ufaransa zinaeleza kuwa klabu ya PSG ipo mbioni kumrejesha aliyekuwa kinda wao Xavi Simons raia wa Uholanzi aliyetolewa kwa mkopo RB Leipzig ya ligi kuu Ujerumani ikiwa Kylian Mbappé ataondoka Paris msimu wa joto.
Tetesi za usajli kutoka nchini Ufaransa zinaeleza kuwa klabu ya PSG ipo mbioni kumrejesha aliyekuwa kinda wao Xavi Simons raia wa Uholanzi aliyetolewa kwa mkopo RB Leipzig ya ligi kuu Ujerumani ikiwa Kylian Mbappé ataondoka Paris msimu wa joto. Mbappe mapema wiki hii aliululisha uongozi wa timu hiyo kuwa ataondoka mwishoni mwa msimu huu huku duru mbalimbali za habari zikimhusisha na klabu ya Real Madrid moja kwa moja.