Kylian Mbappé anakuwa mchezaji mpya wa Real Madrid baada ya kukamilika hatua zote za kusaini NYARAKA za mkataba wake. Real Madrid inajiandaa kumtangaza nyota huyo raia wa Ufaransa kama mchezaji mpya klabuni hapo wiki ijayo.
Huu ni uhamisho ambao Mbappe amekuwa akiota tangu akiwa mdogo wakati ambapo alikuwa akibandika mabango ya gwiji wa zamani wa Real Madrid Cristiano Ronaldo kwenye ukuta wa chumba chake cha kulala.
Ni uhamisho ambao unaweza hatimaye kumletea mataji makubwa zaidi kwenye soka, ni uhamisho ambao unaweza kumfanya kuwa mwanasoka aliyepambwa zaidi wakati wote. Hatimaye ndoto imetimia.