Fri, 8 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbabe wa Yanga SC, CR Belouizdad leo naye atakuwa dimbani kuchuana na mbabe wa Afrika, Al Ahly.
Al Ahly leo atakuwa nyumbani kumualika Belouizdad aliyetofautiana naye alama moja tu kwenye msimamo wa kundi lao, Kundi D.
CR alimfunga Yanga 3-0 kwenye mechi ya mzunguko wa kwanza kisha naye akafungwa na Medeama 2-1 katika mechi ya mzunguko wa pili.
Msimamo wa kundi lao, Al Ahly anaongoza akiwa na alama 4 akifuatiwa na CR mwenye alama 3 kisha Medeama ambaye naye ana alama 3 huku Yanga akiburuza mkia akiwa na alama 1.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live