Wed, 8 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji Jean-Philippe Mateta amepewa tuzo ya mchezaji bora wa msimu wa Crystal Palace.
Mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji waliofunga bao katika ushindi wa Palace dhidi ya Manchester United mwanzoni mwa wiki hii.
United ilikutana na kisago cha mabao 4-0 kutoka kwa Palace katika Uwanja wa Selhurst Park na mchezo huo ulichezeshwa na mwamuzi Jarred Gillett.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live