Thu, 30 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club imefanya mazoezi yake ya mwisho kuelekea mchezo wao wa Ligi kuu dhidi ya wenyeji timu ya Dodoma Jiji.
Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes itakipiga siku ya Ijumaa Oktoba 1 na wataingia katika mchezo huo wakiwa na kumbu kumbu ya kutoa sare katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Kagera.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri Dodoma ambako wenyeji wametoka kubeba pointi tatu dhidi ya Ruvu Shooting.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live