Mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele na winga Jesus Moloko wanaweza kuukosa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons baada ya kushindwa kufanya mazoezi na wenzao huku mazoezi ya leo jioni yatatoa majibu iwapo watakuwa sehemu ya mchezo wa kesho utakaochezwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Saa 1:00 Usiku
Mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele na winga Jesus Moloko wanaweza kuukosa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons baada ya kushindwa kufanya mazoezi na wenzao huku mazoezi ya leo jioni yatatoa majibu iwapo watakuwa sehemu ya mchezo wa kesho utakaochezwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Saa 1:00 Usiku "Dickson Job ana adhabu hatakuwepo kwenye mchezo wa kesho, Jesus na Mayele hawajafanya mazoezi tutawaangalia kwenye mazoezi ya leo kama watatumika kwenye mchezo wa kesho ila Morrison na Mwamnyeti wamerudi mazoezini lakini bado hawako vizuri asilimia mia moja," amesema kocha msaidizi wa Yanga Cedric Kaze