Thu, 8 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya jana klabu ya Pyramids ya Misri anayoichezea mshambuliaji Mayele Fiston kütangaza kuachana na kocha Jaime Pacheco, rasmi klabu hiyo leo imetangaza kumchukua Krunoslav Jurcic kuwa mkuu wa kikosi hicho.
Uamuzi wa kumtangaza kocha Jurcic raia wa Croatia, umekuja kufuatia kuondolewa kwa kocha Pacheco aliyekuwa na matokeo mabaya na kikosi hicho.
Mechi ya kwanza ya kocha huyo inatarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii katika mchezo wa Ligi Kuu ya Misri, ambapo kikosi chake kitacheza dhidi ya ZED FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live