Thu, 14 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Azam imempa ofa ya mshahara wa zaidi ya sh milioni 38 za Kitanzania kwa mwezi na ada ya usajili ya ya milioni 300 mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo na Pyramid FC, Fiston Mayele ili asaini mkataba wa miaka miwili mwisho wa msimu.
Azam wanasaka mbadala wa Prince Dube ambae ameachana na Klabu hiyo wiki chache zilizopita.
Wakati huo huo Prince Dube anatajwa kujiunga na Yanga ambao kwa muda mrefu wanasaka Straika atakaeziba nafasi ya mayele baada ya wote walioletwa kuonekana wameshindwa kuvaa viatu vyake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live