Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maxi Nzengeli aapa kuvunja rekodi Ligi Kuu

Maxi Nzengeli X Congo Kiungo wa Yanga, Maxi Mpia Nzengeli

Thu, 12 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo fundi wa boli, Maxi Nzengeli alisema anaendelea kuizoea ligi ya Tanzania akitaka kuvunja rekodi aliyoanza nayo ya kufunga na kuasisti kwa timu hiyo iliyomsajili kutoka AS Maniema ya DR Congo. Maxi anasema msimu uliopita katika ligi ya DR Congo hadi iliposimama alitengeneza asisti tatu na kufunga manne katika mechi nane Maniema.

“Ninapocheza kama kiungo jukumu langu kubwa ni kuzalisha pasi za mabao hili ndio nataka liwe linatangulia kwangu hizi mbili ni chache sana nataka kutoa pasi za mabao zaidi kuliko kufunga,” alisema Maxi na kufichua kuwa mzuka unaomfanya kufanya makubwa uwanjani ni umati wa mashabiki ambao wapo kila wanakokwenda.

“Hapa watu wanapenda sana mpira, kila unapokwenda unakutana na mashabiki wengi. Tena, sisi tunasafiri na ndege lakini wako mashabiki wengine wanasafiri kwa umbali mrefu kwa mabasi. Hawa ndio wanatufanya tuongeze juhudi uwanjani,” alisema.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: