Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mauya bado yupo sana Yanga

Mauya Sign.jpeg Mauya bado yupo sana Yanga

Sun, 16 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo Zawadi Mauya ataendelea kuwatumikia Wananchi baada ya makubaliano ya kuongeza mkataba wa mwaka mmoja kufikiwa

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga imebainisha kuwa Kocha Miguel Gamondi amependekeza Mauya aongezwe mkataba baada ya mkataba wake wa awali kumalizika

Ni baada ya Muargentina huyo kujiridhisha hakuna wachezaji wengi wa ndani wanaocheza nafasi ya Mauya ambao ni bora kuliko yeye

Yanga huenda isiwe na ingizo jipya kwenye safu ya kiungo cha ukabaji ambapo Mauya, Jonas Mkude, Khalid Aucho, Mudathir Yahya na Salum Abubakar 'Sure Boy' wataendelea kuhudumu katika eneo hilo

Aidha, imeelezwa Gamondi amependekeza usajili wa wachezaji wanne kuongeza nguvu katika maeneo ya safu ya ulinzi (pembeni), winga na eneo la ushambuliaji

Chanzo: www.tanzaniaweb.live