Mon, 20 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakala wa Matthijs de Ligt, Mino Raiola amethibitisha kuwa mteja wake anatamani sana kuondoka Juventus na kupata changamoto mpya msimu ujao.
Juventus walimpata nyota huyo wa Uholanzi mwaka wa 2019, na tangu wakati huo ameichezea klabu hiyo mara 94 katika mashindano yote.
Wakala wa De Ligt amethibitisha kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 yuko tayari kwa hatua mpya, na akafichua kuwa huenda mpango kuelekea Ligi ya Premia uko kwenye ajenda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live