Mon, 11 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Msaidizi wa Simba SC, Selemani Matola amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenye mechi yao ya kesho dhidi ya Singida FG na kwamba wao wamejipanga kuwapa furaha.
Matola ameyasema hayo alipokuwa kwenye mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wao huo wa kesho ambapo alisema, wanafahamu ubora wa Singinda na wamejipanga ili kuwakabili.
"Tumekuwa tukipata wakati mgumu sana kila tunapokutana nao Singida, tunafahamu ni wagumu sana lakini sisi tumejipanga kuwapa furaha mashabiki wetu," alisema Matola.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live