Thu, 9 Nov 2023
Chanzo: Tanzania
Kaimu Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola, amesema amefurahishwa na morali ya wachezaji kuelekea mchezo wao dhidi ya Namungo unaotarajiwa kuchezwa leo Novemba 9, 2023 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar.
Matola ameyasema hayo alipokuwa kwenye mazoezi ya mwisho ya Simba katika uwanja wa MO Simba Arena Bunju ambapo amesema, mashabiki wasahau kuhusu mchezo wao dhidi ya Yanga kwani umeshapita.
"Niwaambie tu wanasimba, twendeni kwenye mchezo wetu wa kesho (leo) dhidi ya Namungo FC, mchezo ule umeshapita tusahau na tukaisapoti timu yetu," alisema Matola.
Chanzo: Tanzania