Sun, 10 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi ya Championship jana Oktoba 9 imeengia katika hatua ya raundi ya pili ambapo viwanja mbali mbali viliwaka moto.
Vinara wa Ligi timu ya DTB, ilishuhudia ikivutwa shati na kulazimishwa sare ya magoli 1-1 na timu ya Green Warriors huku wakishuhudia mshambuliaji wake Amisi Tambwe alishindwa kumaliza mchezo baada ya kufanyiwa madhambi.
Hali kadhalika timu ya African Sports imetoa kipigo kizito cha magoli 4-0 dhidi ya Mwadui FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live