Wed, 17 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mataifa 10 ya Afrika yamefuzu kwa hatua ya mtoano kwa ajili ya kupata Mataifa matano yatakayoiwakilisha Afrika katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Qatar 2022.
Timu hizo 10 zilizofuzu zitacheza mechi nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndio atakaepita kupata timu tano zitakazokwenda Qatar.
Timu hizo 10 zilizofuzu ni pamoja na DR Congo, Mali,Nigeria, Tunisia, Algeria, Ghana, Cameroon, Morocco, Misri na Senegal.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live