Ushindani utakuwepo kwa sababu Simba inapokuwa kwenye mashindano ya kimataifa hawawi wanyonge! Lakini kwa mwendo wao wa msimu huu Kocha Robertinho anahitaji kufanya mabadiliko makubwa ili kuleta ushindani kwenye mchezo huo wa Oktoba 20, 2023.
Isitegemewe historia peke yake kwamba Simba imeshaifunga Al Haly mara mbili kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, mabadiliko lazima yaanzie kwenye benchi la ufundi na wachezaji kujituma uwanjani.
Al Ahly tulivyoiona na namna walivyonza Ligi ya mabingwa msimu huu pamoja na Ligi yao, bado naona Ahly ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri dhidi ya Simba kwenye mchezo wa kwanza Oktoba 20, 2023.