Kelele za kwamba timu haichezi vizuri huwenda zikawa hazina maana kama tu, mashabiki wataingalia timu yao kwa jicho la takwimu kwani mpaka sasa, Simba ina un beaten 29 katika mechi za Ligi Kuu ya NBC.
Hii inatokana, tangu Roberto Oliviera 'Robertinho' atue Msimbazi katika dirisha dogo la usajili mapema mwaka huu, hajapoteza mchezo wowote wa Ligi Kuu.
Juzi alipocheza mchezo wake wa raundi ya saba dhidi ya Ihefu, ndipo alipofikisha un beaten hiyo na Jumapili hii anakwenda kucheza dabi yake na Yanga SC mchezo wa raundi ya nane akiwa na alama zake 18 sawa na Yanga anayeongoza Ligi.
Hata hivyo, Simba anacho kiporo kimoja mkononi cha mchezo wa raundi ya sita dhidi ya Mashujaa.