Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mastaa Yanga waahidi ushindi mbele ya Ihefu

Mudathir Yahya Press Kiungo wa Yanga, Mudathir Yahya

Tue, 3 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo wa Yanga Mudathir Yahaya amesema kuwa mchezo wa kesho Oktoba 4 dhidi ya Ihefu wameahidi kwenda kuchukua alama tatu ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea Ubingwa wao.

Yanga ambao msimu uliopita waliacha alama tatu na kuvurugiwa rekodi yao ya "Unbeaten" wana kumbukumbu mbaya katika Uwanja wa Hingland Estate lakini wamesema kuwa safari hii hakuna kikwazo cha kushindwa kuchukua alama tatu.

Akizungumza Kiungo huyo katika Mkutano wa Waandishi wa Habari amesema;

"Kwa niaba ya wachezaji wenzangu napenda kuchukua fursa hii kwanza kumshukuru mwenyezi Mungu tumefika salama na tumekuja hapa kupambana na kuhakikisha tunaondoka na alama tatu kwenye mchezo wetu wa kesho"

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: